WATENDAJI WA VIJIJI WATAKIWA KUANDAA MIPANGO MAALUM YA KILIMO

 
SERIKALI wilayani Bunda mkoani Mara,imewaagiza viongozi wenyeviti na watendaji wa vijiji vyote vya wilaya hiyo, kuandaa mipango maalum ya kilimo kwa kuanda madaftari ya kuorodhesha mashamba ya kila kaya katika kuhakikisha wilaya hiyo sasa inaondokana na tazizo la njaa linalojitokeza mara kwa mara.
 
Mkuu wa wilaya ya Bunda Bw Joshua Mirumbe,amesema tayari viongozi hao wa vijiji,wameagizwa kuandaa madaftari hayo ambayo yatatumika kuorodhesha mashamba ya mazao ya chakula na biashara kwa kila kaya kuanzia sasa.
 
Kwa sababu hiyo mkuu huyo wa wilaya ya Bunda,amesema  Serikali kamwe haitasita kuwakamata na kuwafungulia mashitaka viongozi hao wa vijiji watakashindwa kutekeleza agizo hilo na kuweka mipango  mizuri ya kufanikisha kilimo ambacho pia kinalenga kuinua uchumi wa wananchi.
 
Hata hivyo mkuu huyo wa wilaya ya Bunda, amesema serikali wilayani humo imeanzisha utaratibu wa kupima utendaji wa kila kiongozi wa kijiji kwa jinsi anavyojishughulisha na utatuzi wa kero zinazowakabili wananchi katika eneo lake  pamoja na kutanguliza mbele utawala wa  bora unazingatia sheria na kwamba atakaeshindwa kufanya hivyo ni vyema akajiondoa mwenyewe katika nafasi hiyo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo