WANANCHI wa mji wa Nyamongo Wilayani Tarime
Mkoani
Mara,wamelaani kitendo cha askari wa jeshi la polisi kutumia nguvu kubwa
kwa
kuwapiga mabomu na risasi za moto wananchi wanaokota mawe katika mgodi
wa
ABG North Mara jambo linalosababisha mauaji na vilema vya kudumu kwa
wananchi.
Wamesema kuwa polisi hawapaswi kufanya vitendo
hivyo
vya mauji ya wananchi kwakuwa baadhi yao ni miongoni mwa watu wanahusika
na
vitendo hivyo vya wizi huo wa mawe katika mgodi huo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti,wanasema ni
kweli
wananchi wamekuwa wakiingia katika maeneo ya mgodi huo kwaajili ya
kuokota
mabaki yam awe lakini pia polisi wanakuwa zamu wamekuwa wakibariki
vitendo
hivyo kwa kupewa fedha na wananchi.
Wamedai kuwa mbali na polisi hao kupewa fedha
na
kuruhusu wananchi kuingia ndani ya mgodi kabla ya kutofautiana na kuanza
kuwashambulia kwa mabomu pia wamekuwa wamekuwa wakiiba mawe ya dhahabu
ndani ya
mgodi kisha kuyuza kwa wananchi.
Mmmoja ya wananchi hao Bw Chacha Mwita mkazi
wa
Nyangoto,amesema kuwa kitendo cha wananchi kuingia mgodini ni baada ya
kupatiwa taarifa na askari polisi wanaolinda mgodi mara tu dhahabu
inapoonekana
ambapo wananchi uwapatia pesa nakuwaruhusu kuingia mgodini.
Kamanda wa polisi mkoa kanda maalum ya Tarime
na Rorya
ACP JUSTUS KAMUGISHA,amekiri kupata taarifa hizo lakini amesema hakuna
mwananchi anajitokeza hadharani kuwataja polisi hao ili hatua kali za
kinidhamu
na kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yao.
