UBUNIFU BADO UNAHITAJIKA ILI KUPATIWA UFADHILI WA MIRADI MBALIMBALI

Imebainika kuwa miradi mingi inayoibuliwa na halmashauri/asasi mbalimbali na kuhitaji ufadhili wahisani mbalimbali inashindwa kupatiwa ufadhili kutokana na wengi wao kuandika kuwa watatoa mafunzo kuliko vitu vingine vya ziada ambayo vitatatua changamoto hizo

Kutokana na wengi kuandika kuwa watatoa mafunzo kwa watu mbalimbali badala ya kuainisha njia nyingine za ziada za kutatua changamoto zinazoikabili jamii, njia hiyo imeonekaka kuwakera wahisani na kuona kuwa hakuna jipya litakalojitokeza katika changamoto hizo pindi watakapotoa ufadhili

Akizungumza kwenye kikao cha kuandaa mikakati ya namna wilaya ya Makete itatokomeza maambukizi ya virusi vya UKIMWI kwa wananchi wake, Bi Alice kutoka shirika la umoja wa mataifa la kuhudumia watoto ulimwenguni (UNICEF), amesema haikatazwi mipango hiyo kuwa na kipengele cha kutoa mafunzo ili kukabiliana na changamoto husika, lakini kinavyokuwa kikubwa inapelekea wafadhili kuwa na hofu ya kufanya nao kazi

“Wakati mwingine zile trainings (mafunzo) zikiwa kubwa katika majadiliano wafadhili hawaipi kipaumbele kabisa yaani wataifanya ya mwisho, na kama zipo fedha basi watafadhili, kwa sasa tutazame zaidi njia nyingine za kufanya achilia mbali mafunzo” alisema bi Alice

Amsema umefika wakati kwa sasa kuhakikisha kuwa waandikaji wa mikakati mbalimbali wahakikishe wanaainisha njia mbadala ambazo zitamvutia mfadhili kuweza kufadhili zitakazotumika kutatua changamoto zilizopo kwa jamii


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo