MKUU WA WILAYA YA MAKETE AWATAKA AMBAO HAWAJAHESABIWA MAKETE KUTUMIA NAFASI ILIYOONGEZWA NA SERIKALI VIZURI



Wananchi wilayani Makete ambao hawajahesabiwa katika zoezi la sensa ya watu na makazi lililoanza Agosti 26 mwaka huu wametakiwa kutoa taarifa zao kwa wenyeviti wa vijiji ama vitongoji vyao ili waje kuhesabiwa katika muda ulioongezwa na serikali

Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Makete ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya sensa wilaya ya Makete wakati akizungumza kwenye kikao cha kamati ya sensa wilaya ofisini kwake

Amesema katika kipindi hiki ambacho serikali imeongeza muda wa kuhesabiwa hadi Septemba 8 ni vyema wananchi hao wakatoa taarifa kwa viongozi wao wa vitongoji ama vijiji ili utaratibu wa kuwafuata walipo ili wahesabiwe ufanyike mara moja

Amewataka wananchi hao kutosita kutoa taarifa hizo katika kipindi hiki na kuwa muda hautaongezwa tena zaidi ya hapo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo