Wakulima wa zao la Pamba wa kjijiji cha Kihumbu
katika kata ya Hunyari wilayani
Bunda mkoani Mara,wamelazimika kuyazuia malori yanayosomba pamba kutoka
katika
maghala ya kijiji hicho kwa madai ya wanunuzi wake kushindwa kuwajalipwa
fedha
zao baada kuwazia pamba yao kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa.
Wakisimulia mkasa huo kwa mbunge wa jimbo la Bunda Mh Stephen Wasira,wakati wa mkutano wa hadhara ambao umefanyikia kijijini hapo, wakulima hao wamesema wamelazimika kuchukua uamuzi huo baada ya kuhofia kuwa pamba yao ambayo wameyauzia makampuni hayo ingechukuliwa bila malipo.
Wakisimulia mkasa huo kwa mbunge wa jimbo la Bunda Mh Stephen Wasira,wakati wa mkutano wa hadhara ambao umefanyikia kijijini hapo, wakulima hao wamesema wamelazimika kuchukua uamuzi huo baada ya kuhofia kuwa pamba yao ambayo wameyauzia makampuni hayo ingechukuliwa bila malipo.
Wamesema wamesema kabla ya kufikia hatua hiyo ya kuzuia magari ya kampuni hizo walipiga yowe na baada ya kukusanyika walifanya maandamano hadi kwene eneo la maghala hayo na kuanza kupanga mawe kwaajili ya kuzuia kuondoka kwa magari hayo.
Makampuni yanayodaiwa kununua pamba kwa mkopo kijijini hapo ni S&C
Ginneries,Olam(T) limited na Alliance Ginneries Ltd ambayo hata hivyo haijajulikana kiasi halisi cha fedha kinayodaiwa ingawa mwenyekiti wa
kijiji hicho Bw Kitenta Thomas, amesema zaidi ya wakulima 200 ndio wanaodai fedha hizo.
Kwa upande
wake Mh Wasira ameonesha kusikitishwa na kitendo cha wanunuzi wa zao la
pamba kuwakopa wakulima kinyume na maelekezo ya mkataba wa ununuzi na
kuyataka yaache mara moja kufanya hivyo kwani ni kuvunja sheria huku
akiwaasa
wakulima kutokopesha mazao yao kwa namna yoyote ile.