MUSOMA
MBUNGE wa Jimbo la Musoma Mjini Vincent Nyerere
amesema kuwa hakuna Mfanyabiashara yeyote atakayeondolewa katika eneo la
Soko
la Mwigobero bila kuonyeshwa sehemu nyingine ya kufanyia biashara
hiyo.
Akiongea kwa njia ya Simu kutoka Jijini Dar es
Salaam,Mh Nyerere amesema kuwa zipo taarifa kuwa Wafanyabiashara
hao wanatakiwa kuondoka katika
Eneo hilo la Soko la Mwigobero kupisha ujenzi wa soko la kisasa kwa
ushirikiano
na Mamlaka ya Bandari.
Amesema Wafanyabiashara wote waliopo katika eneo
hilo hawataondoka eneo hilo bila kupewa eneo lingine,amesema
Wafanyabiashara
hao watapata Vibanda sehemu watakayotengewa hivyo waondoe wasiwasi.
Naye Mstahiki Meya wa Manisspaa yaa Musoma Alex
Kisurura amesema kuwa tayari Mamlaka ya
Bandari imetoa fidia kwa wafanyabiashara 46 walikuwa ndani ya soko hilo wakati
wa Tathimini.
Kwasababu hiyo Mstahiki Meya amesema kuwa wananchi wa eneo hilo la
Mwigobero hawapaswi kuwa na hofu katika kufanyabiashara katika eneo hilo
na
hivyo kuwataka wafanyebiashara zao kwa amani.
Kauli za Viongozi hao zinafuatia
malalamiko yaliyotolewa na Baadhi ya wafanyabiashara katika Soko hilo
ambao walisema kuwa kumekuwepo na kutokuwa na Uwazi katika Mchakato wa
Ujenzi wa Soko hilo huku Wafanyabiashara hao wakisema hawajui wapi
watakapoenda kufanya biashara zao
Eneo la soko la Mwigobero
linatarajiwa kujengwa
kisasa kwa mujibu wa Viongozi hao ambapo Manispaa ya Musoma
itashirikiana na
Mamlaka ya Bandari kufanikisha Ujenzi huo