AJERUHIWA NA MAJAMBAZI, NA KULAZWA HOSPITALI AKIWA HOI

 
MKAZI mmoja wa kijiji cha Maneke katika kata ya Tegeruka wilaya ya Butiama, Bw Magwegwe Chiriso amelazwa katika hospital ya mkoa wa Mara baada ya kuvamiwa na watu wanaosadikiwa kuwa majambazi na kisha kumpora kiasi cha shilingi laki tisa.
 
Akizungumza katika wodi namba 8 ya hosptali hiyo mjini Musoma majeruhi huyo amesema kuwa tukio hilo limetokea juzi majira ya saa 6 usiku baada ya watu hao kuvunja mlango wake kwa kutumia jiwe kubwa maarufu kama Fatuma.
 
Amesema kuwa baada ya majambazi hao kubomoa mlango huo waliingia ndani  majambazi wawili wakiwa na silaha za jadi ambapo walimuamilisha yeye na mke wake wake wawape pesa kiasi cha shilingi laki saba huku wakiwakata kata kwa mapanga.
 
Amefafanua kuwa baada ya kuona wanazidi kushambuliwa zaidi aliwaonyesha fedha hizo zikiwa sandukuni hivyo kubobomoa kwa kutumia vyuma kisha kuchukuwa kiasi cha shilingi laki tisa na kutokomea kusikojulikana.
 
Amesema kuwa baada ya kuona wameondoka yeye na mke wake walipiga yowe ambapo majirani walifika na kuwachukuwa hadi katika kituo cha polisi Musoma ambako walipewa fomu namba 3 na kisha kwenda kutibiwa katika hospital hiyo ambako amelazwa yeye na mke wake.
 
Akizungumzia tukio hilo kwa niaba ya kamanda wa polisi wa mkoa wa Mara,mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai mkoa wa Mara Bw Emanuel Lukula amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kudai kuwa polisi bado wanaendelea na uchunguzi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo