WATANO WAHUKUMIWA JELA MIAKA 52


WATU watano wakazi wa kijiji cha Makilawa kata ya Minyughe wilayani Singida, wamehukumiw na mahakama ya wilaya adhabu ya kutumikia jumla ya miaka 52, baada ya kupatikana na hatia ya kuvunja mlango wa duka la Jisaba Jaji, na kisha kuiba mali na fedha tasilimu, vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 2,168,000.

Washitakiwa hao waliopewa adhabu hiyo ni Hasan Jumanne, Rashid Mwela Mwanga na Seif Ismail Nguru, ambao kila mmoja atatumikia jela miaka 14.

Washitakiwa wengine ni Abdallah Masoud Iboma na Jumanne Mjoi@Banka. Hawa watatumika jela kila mmoja miaka 10.

Mapema mwendesha mashitaka mwanasheria wa serikali, Mary Mdulungu, alidai mbele ya hakimu wa mahakama hiyo, Flora Ndale kuwa mnamo Julai 13 mwaka jana saa 4:30 usiku huko kijiji cha Makilawa, washitakiwa kwa makusudi walivunja mlango wa duka mali ya Jisaba Jaji, na kuiba mali mbali mbali na fedha taslimu 300,000/=.

Alisema pamoja na fedha hizo taslimu, washtakiwa waliiba sola moja aina ya sujo, simu tano aina ya nokia, pea 85 za vitenge na pesa 104 za khanga.

Mdulungu alitaja mali nyingine iliyoibwa ni katoni mbili za betri aina ya tiger na dazani mbili ya perfume mali yote hiyo pamoja na fedha taslimu shilingi 300,000, thamani yake ni shilingi milioni 2,168,000.

Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo, mwanasheria wa serikali, Mdulungu, aliiomba mahakama hiyo, itoe adhabu kali kwa washitakiwa ili iwe fundisho kwao na kuogofya watu wengine wanaotarajia kutenda aina ya makosa ya wizi na unyang’anyi.

Kwa upande wao washitakiwa kila mmoja kwa nafasi yake, waliiomba mahakama hiyo iwape adhabu nafuu. 

Wakati huo huo, mahakama hiyo ilimwachia huru kasimu Ramadhani baada ya upande wa mashitaka kushindwa kumuunganisha na shitaka hilo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo