MUUNGANO
wa
vilabu vya waandishi wa habari nchini UTPC, umenza kutoa mafunzo maalum
kuandika habari za afya kwa waandishi wa habari katika mikoa yote
nchini.
Hatua
hiyo
inalenga kuwajengea uwezo waandishi wa habari kuandika habari za afya
zilizofanyiwa utafiti wa kina kwa lengo la kuboresha sekta afya na
kufikisha ujumbe sahihi kwa jamii.
Mkurugenzi
wa
UTPC Bw Aboubakar kassan, ameyasema mjini Musoma wakati wa mafunzo ya
kwanza ya
siku nne kuanza kutolewa nchini kwa waandishi wa habari mkoani Mara
ikiwa ni
sehemu ya utatuzi wa matatizo na kuibua changamoto zinazokabili utoaji
wa huduma
ya afya nchini.
Amesema
kwa muda
mrefu jamii imekuwa ikikabiliwa na sintofahamu juu ya kujikinga na
maambukizi
ya magonjwa hususan Ukimwi kutokana na waandishi nchini kutoandika
habari
ambazo zimefanyiwa utafiti wa kina ambao haotoi majibu ya namna ya
kujikinga na maambukizi mapya.
Kwa
sababu hiyo
ametoa wito kwa wanahabari mkoani Mara kutumia vema nafasi ya mafunzo
hayo kwa
lengo la kuibua changamoto zinazokabili sekta ya afya hasa maeneo ya
vijijini
ili kuwezesha wananchi kutumia mbinu bora za kujikinga na maradhi.
Kwa
mujibu wa
mwezeshaji wa mafunzo hayo DK Ahmed Twaha,amesema takwimu za kiafya
hususan
katika maeneo ya vijijini zinaonesha kuwa zaidi ya asilimia 60 ya
wagonjwa
wanaofika katika vituo vya afya ni wanawake na watoto hivyo wanahabari
wanapaswa kuibua mbinu kadhaa ya kunusuru kundi hilo kwa kuripoti njia
bora za
kujikinga na maambukizi ya maradhi kama vile Ukimwi na Malaria.
