MKUU wa Wilaya ya Muheza, Subira Mgalu amewataka wazazi wa wanafunzi wa shule za msingi za Tarafa ya Amani Wilayani hapa kuwa na ada ya kufuatilia maendeleo ya watoto wao mashuleni pamoja na kupiga vita mimba za utotoni.
Akizungumza kwa
nyakati tofauti juzi
katika vijiji mbalimbali vya Tarafa ya Amani wakati wa uhamasishaji wa
wananchi
kushiriki kikamilifu katika zoezi la Sensa ya watu na makazi, Mgalu
alisema
kuna baadhi ya wazazi wamekuwa wakijisahau umuhimu wa elimu kwa watoto
wao.
Alisema Serikali
imekuwa ikijitahidi
kuhakikisha kila mtoto anapata elimu ya msingi hadi ya sekondari bure na
hivyo
ni wazazi kufuatilia maendeleo ya mtoto wao lengo likiwa ni kupata elimu
stahiki
ambayo itamsaidia katika maisha yake ya baadae.
Alisema kuna baadhi
ya wazazi
wamekuwa wakiwashirikisha watoto wao katika kazi za kijamii pamoja na
kilimo
wakati wa masomo jambo ambalo linachangia kwa kiwango kikubwa kumfanya
mtoto
kutopenda shule.
“Ndugu zangu wa
Tarafa ya Amani na
vitongoji vyake muliopo hapa kunisikiliza, nimepata taarifa kuwa huku
kuna
tatizo la utoro wa wanafunzi na mimba shuleni, hivyo natoa onyo kuwa
nimekuja
kimapambano” alisema Mgalu
Mgalu alisema
amekuja katika Wilaya
hiyo kushirikiana na wananchi wa Muheza katika suala zima la maendeleo
ikiwa na
pamoja na kuleta umoja na mshikamano katika jamii huku akiwa na taarifa
za
kukithiri kwa mimba mashuleni jambo ambalo amedai atalivalia njuga.
Alisema suala hilo
limekuwa
likimuumiza kichwa na kumnyima usingizi na kuahidi kulifuatilia ili
kukomesha
vitendo hivyo na moja ya mbinu ambazo atazitumia ni kuitisha vikao vya
wazazi
na walimu na kupanga mikakati ili kuhakikisha mimba na utoro mashule
unatokomea.
Alisema chanzo cha
watoto kubeba
mimba utotoni na kuacha masomo shuleni inasababishwa na wazazi majumbani
ikiwa
na pamoja na malezi hivyo ni vyema kuitisha vikao vya walimu na wazazi
na
kuweza kujadili namna ya kuweza kuondosha tatizo hilo.
Alisema ikiwa
wazazi watakuwa na
ushirikiano mzuri na walimu ikiwa na pamoja na wanafuzi wao tatizo la
mimba na
utoro mashuleni linaweza kuondoka na kuifanya Wilaya hiyo kufanya viruri
katika
ufaulu wa wanafunzi katika mitihani ya kitaifa.