WANANCHI CHUKIENI RUSHWA NA UKABILA

Na Augustine Mgendi, BUTIAMA
WATANZANIA wametakiwa kuchukia vitendo vya rushwa,ubaguzi,ukabila,udini  na ubinafsi ili kulinda amani ya nchi ikiwa ni njia moja wapo ya kumuenzi kwa vitendo baba wa taifa Hayati Mwalimu Julius Kabarage Nyerere.
Hayo yamesemwa kijijini Butiama mkoani Mara na kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka huu Bw Honest Ernest Mwanonossa,mbele ya kaburi la baba wa taifa, baada ya kuwasha Mwenge wa Mwitongo nyumbani kwa baba wa taifa hayati mwalimu Julius Kambarage Nyerere  katika eneo la Mwitongo.
Amesema kuna baadhi ya viongozi nchini wameshindwa kumuenzi Baba wa taifa kwa kukemea kwa vitendo matumizi ya  ukabila,udini na rushwa hasa katika siasa jambo ambalo ni hatari na kwamba vitendo hivyo visipothibitiwa mapema vinaweza kuhatarisha amani ya nchi.
Akiwa kijijini Butiama, kiongozi huyo wa mbio za mwenge  kitaifa,ameweka jiwe la msingi katika jengo la wodi ya wazazi na watoto ambalo linajengwa kwa ushirikiano wa wananchi wa kijiji cha Butiama,Halmashauri  ya Musoma vijijini na Serikali kuu kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 483 kama sehemu ya kuongeza miundo mbinu katika hospitali hiyo inayotarajiwa kuwa ya wilaya mpya ya butiama.
Awali viongozi hao wakiongozwa na kiongozi huyo wa mbio za mwenge  kitafa,wamepata fursa ya kuomba na kuweka mashada ya maua katika kaburi la baba wa taifa hayati mwalimu Julius Nyerere.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo