Bwawa la nyumba ya Mungu
Na Belinda Semtandi, MOSHI
BODI ya maji bonde la pangani imesema
kufuatia
hali ya maji katika bwawa la nyumba ya mungu kupungua sana kutokana na
kukosekana na kwa mvua za masika na uharibifu wa mazingira uzalishaji wa
umeme
katika bwawa hilo uko hatarini kusitishwa
Hayo yamebainishwa na
mwenyekiti
wa bodi ya maji bonde la pangani Julius sarmatt wakati wa mkutano wa
wadau wa
maji kutoka mikoa ya kanda ya kaskazini waliokutana mjini moshi na
kueleza kuwa
hali ya bwawa hilo kwa sasa ni mbaya
Alisema kiwango cha uzalishaji umeme
katika
bwawa hilo umeshuka kutoka megawati 8 zilizokuwa zinazalishwa awali hadi
kufikia megawatt 3 hali ambayo ni hatari na kwamba endapo
hali hiyo itaendelea itasababisha mitambo ya umeme katika bwawa hilo
kushindwa
kuzalisha umeme
Aidha mwenyekiti huyo aliongeza kuwa
upungufu uliojitokeza mwaka huu haujawahi kutokea katika kipindi cha
miaka ya nyuma na kwamba walitegemea endapo mvua za masika zingenyesha
vizuri
kungesaidia kuongeza maji katika bwawa hilo bila mafanikio za kwamba
maji
yanzidi kupungua siku hadi siku.
“ kutokana na upungufu huo tumeanzisha
mpango
wa mkakati wa kuelimisha wananchi juu ya kuanzisha vyama vya usimamizi
wa maji
na kulinda vyanzo vya maji hatua ambazo zitaweza kupunguza tatizo la
maji
katika bwawa hilo”alisema sarmatt
Mapema akizungumza na wadau wa maji
kutokoka
mikoa ya arusha ,Kilimanjaro,manyara,tanga waliokutana mjini moshi
kujadili
utekelezaji wa mpango wa miaka 25 wa usimamizi na endelezaji wa
raslimali za
maji katika bonde la pangani katibu tawala mkoa wa Kilimanjaro Faisali
Issa
alisema kuwa hali ya maji kwa mkoa wa Kilimanjaro ni mbaya
Kutokana na hali hiyo Issa aliwataka
wenye
viwanda na mashamba makubwa ya umwagiliji kuangalia uwezekano wa
kupunguza
matumizi ya maji yasiyo ya lazima ikiwa ni pamoja na kusafisha maji taka
ili
kurudi katika mzunguko hali ambayo itapunguza tatizo la ukosefu wa maji
ambao
umesababisha kuwepo kwa migogoro baina ya wananchi waishio ukanda wa juu
na
wale waishio ukanda wa chini
