WAKULIMA WA KAHAWA MOSHI WALALAMIKIA URASIMU


WAKULIMA wa zao la kahawa katika jimbo la Vunjo wamelalamikia urasimu unaofanywa na taasisi ya utafiti wa kahawa nchini (tacri)kwa kutofikisha huduma zao maeneo mengi ya vijijini ambapo ndipo wakulima wengi wanakopatikana.

Wakulima hao walitoa kilio chao katika mikutano ya hadhara mbele ya mbunge wa jimbo hilo Agustine Mrema na kudai kuwa taaisi hiyo inaonekana kuwanufaisha watu wachache na sio wakulima kama uhalisia wa taasisi hiyo.

Mwenyekiti  wa chama cha msingi cha Mrimbo Uuwo Livingstone Shao alisema kuwa taasisi ya utafiti wa kahawa nchini (TACRI)imekuwa ikiwafanya wakulima walio wengi kushindwa kupata pembejeo au elimu juu ya utunzwaji wa zao hilo.

‘Mh mbunge TACRI tumekuwa tukiisikia tu ila hatujawahi kunufaika na taasisi hii sasa sijui kama inashia mjini kama kutakuwa na wakulima wa zao hili kweli”alisema mwenyekiti huyo

Mbali na taasisi hiyo kutofika maeneo ya vijijini bado walilalamikia kutopatikana kwa miche ya kahawa ambapo hata ikiopatikana huuzwa kwa bei ghali jambo ambalo mkulima wa kawaida anashindwa kumudu.

Mbunge wa jimbo hilo Agustine Mrema aliwataka wakulima hao kuweza kuandika malalamiko yao ili aweze kuyashughulikia na kufikisha katika ngazi husika ili yaweze kutatuliwa na kupatikana kwa suluhu ya kudumu.

Mrema alifanya ziara katika   kata ya Mwika kaskazini na kuweza kuongea na wananchi katika mikutano ya hadhara katika vijiji vya Lole ,na Mrimbo uuwo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo