MKUU WA WILAYA YA KILOLO AWATAKA WASIMAMIZI NA MAKARANI WA SENSA KUTOLIHUJUMU ZOEZI HILO

MKUU wa Wilaya ya Kilolo, mkoani Iringa Gerald Guninita amewaomba wasimamizi na makarani wa zoezi la sensa Wilayani humo kutolihujumu zoezi hilo badala yake wafanye kazi kwa bidii na uaminifu mkubwa.
 
Guninita amelazimika kuwasihi wasimamizi na makarani hao ambao asilimia 90 ni walimu wa shule za msingi na Sekondari kufuatia kuwepo kwa minong’ono kwamba fedha watakazolipwa ni kidogo ikilinganishwa na matarajio waliyokuwa nayo hapo awali.
 
Akifungua mafunzo kwa makarani na wasimamizi hao wa zensa, Guninita alisema Serikali wilayani humo imewateua watumishi wengi wa umma kufanya zoezi hilo kutokana na uvumilivu wao wakati yanapotokea matatizo ya kifedha hivyo, kuwasihi wawe wavumilivu ili matokeo ya kazi yao yaliletee taifa mafganikio.
 
“Nawashukuru sana walimu wa Kilolo ambao hawakuonyesha mgomo wakati wenzao wapo kwenye mgomo, uvumilivu wenu ndiop umetufanya tuwaamini na kuwaingiza kwenye zoezi hili muhimu kwa maendeleo ya kitaifa, fedha zeni zipo na ninachowaomba muwe wavumilivu na mfanye kazi kwa bidii,” alisema Guninita.
 
Alisema matokeo ya kazi yao yatapimwa baada ya kumalizika kwa zoezi hilo, hivyo ni wajibu wao kufanya kazi kwa kufuata kiapo watakachopatiwa kabla ya kulianza zoezi hilo ambalo linatarajia kufanyika wiki mbili zijazo.
 
Alisema serikali inapenda kuona kuwa sensa ya watu na makazi ya mwaka huu inapata mfanikio makubwa ili kuwezesha kupata takwimu muhimu zitakazotumika katika kufanya maamuzi sahihi na kupanga mipango endelevu.
 
“Serikali inaamini kuwa mtatumia juhudi na maarifa katika kufanikisha zoezi la sensa, kwahiyo ifanyeni kazi hii kwa uaminifu kwa kuzingatia viapo watakavyopewa,”Guninita alisema.
 
Awali wakizungumza na mwananchi, sharti la kutotaja majina yao baadhi ya makarani walisema matarajio yao ya awali wakati wakiomba kazi hiyo yamekufa baada ya kuwa watakuwa wakilipwa sh 35,000 kwa siku badala y ash 65,000 ambayo walikuwa wamedokezwa.
 
"Mtumaini yetu yamefifia kwa sababu kiasi hicho cha fedha tutakachokuwa tukilipwa kila siku ndicho kitakachowawezesha pia kugharamia mahitaji yatu mengine ikiwemo malazi kwa wale watakaokuwa mbali na maeneo wanayoishi na chakula, mara ya kwanza tulifikiri tunghelipwa sh 65,000," alisema mmoja wa makarani hao.
 
Pamoja na kulalamikia malipo hayo, makarani na wasimamizi walioanza mafunzo yao Agosti 9, walilalamika kuchelewa kulipwa fedha hizo kwa zaidi ya siku tatu.
 
Akiwahakikishia kulipwa fedha zao zote, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo.Mohamed Gwalima alikiri fedha kwa ajili ya wasimamizi na makarani wanaoshiriki mafunzo hayo kuchelewa.

“Zimechelewa kwa sababu ya mfumo mpya wa fedha wa EPICOR. Lakini tumeshajulishwa za kuwalipa kwa siku tano za mafunzo yenu ziko tayari na nadhani mtalipwa msiwe na shaka, ” alisema.
 
Alibainisha kuwa mfumo wa EPICOR ambao umeanza kutumika hivi karibuni unalenga kudhibiti matumizi hewa au yaliyo nje ya bajeti.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo