TRAKOMA BADO YAWA CHANGAMOTO KWA JAMII YA WATANZANIA


Imebainishwa kuwa ugonjwa wa Trakoma ni moja ya adha kubwa inayosumbua jamii ya watanzania hasa waishio vijijini katika mazingira yasiyoridhisha kwa usafi na ukosekanaji wa maji.
Hayo yamebainishwa na mganga mkuu wa mkoa wa manyara Dr Samuel Ulomi wakati alipokuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa mafunzo ya utafiti wa awali wa ugonjwa wa Trakoma jana  ya siku nne katika ukumbi wa Veta mkoani Manyara.
Alibainisha kuwa ugonjwa wa Trakoma umegundulika kuathiri sana wakinamama pamoja  na watoto walio na umri wa miaka kati ya mwaka mmoja hadi miaka kumi, pamoja na adha ya ugonjwa huo kwa rika hilo watoto,trakoma ni moja ya magonjwayaletwayo upofu katika umri wa miaka 15-60 na zaidi.
Dr  Ulomi  alifafanua kuwa  baada ya utafiti huo lengo ni kuanza mikakati ya udhibiti wa ugonjwa wa Trakoma kwa kutumia mikakati ya usafi katika wilaya zote zitakazogundulika kuwa na ugonjwa kwa kiwango cha zaidi ya asilimia 10%.
Naye mratibu waTaifa wa magonjwa yasiyopewa kipaumbele kutoka wizara ya Afya Dr Upendo Mwingira alieleza kuwa kutokana na hali hiyo shirika la Afya duniani lilipitisha azimio la kutokomeza upofu unaotokana na Trakoma duniani kote ifikapo mwaka 2020,liliundwa mwaka 1999 linaitwa Global elimination of Trakoma by the year 2020.
Aliongeza kuwa wizara ya Afya na stawi wa jamii,jamuhuri ya muungano ya Tanzania iliridhia azimio hilo la shirika la afya ulimwenguni na kupanga mikakati mbalimbali ya udhibiti wa ugonjwa wa Trakoma nchini.
Aidha alisema kuwa kwa ushirikiano na shirika la International Trakoma initiative(ITI)katika miaka ya 2004-2006 ulifanyika utafiti wa awali wa ugonjwa wa Trakoma katika wilaya 50 ambazo ziligundulika kuwa ugonjwa huo kwa viwango mbalimbali na mikakati ya udhibiti wa ugonjwa huo.
Kwa upande wake meneja wa mradi wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele mabusha,matende,vikope,trakoma,kichocho,minyoo ya tumbo,usubi kutoka shirika lisilo la kiserikali(NGO)IMA  world  health Dr Deogratias Damas alisisitiza kuwa hadi kufikia mwaka 2012 jumla ya mikoa 13 zinatekeleza mpango huo NTD hapa nchini.
Alisema kuwa katika mpango mkakati wa miaka mitano wa NTD moja ya kipaumbele ni kukamilisha utafiti wa awali katika wilaya ambazo hazikufanyiwa utafiti na kwa mwaka huu wizara,wadau wanatekeleza kazi hii ya tathmini ya awali katika wilaya 10 na pia utafiti wa ufuatiliaji katika wilaya tatu.
Katika mafunzo hayo washiriki  ni kutoka wilaya Babati pamoja na wilaya ya Mbulu wizara ya afya imeshirikisha wilaya hizi katika utafiti huo wa awali wa ugonjwa wa Trakoma na mada zilizotolewa ni vikope lengo mkakati wa kupambana na ugonjwa wa vikope malengo ya kuangalia kiwango cha maambukizi ,namna ya kufanya utafiti kwa kuangalia ugonjwa wa vikope.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo