Imesemekana
kuwa zoezi la Sensa katika Wilaya ya Babati na halmashauri ya mji wa
Babati mkoa wa Manyara,huenda likashindwa kufanikiwa kutokana na baadhi
ya
vifaa kupungua ama kuisha wakati zoezi hilo likiwa linaendelea.
Taarifa
hiyo imetolewa na Mratibu wa sensa wa Halmashauri ya mji wa
Babati,Bw.John Malle katika kikao cha wajumbe wa kamati ya Sensa ya
wilaya
kilichofanyika jana katika Ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Babati
mkoani Manyara.
Alibainisha
kuwa kwa upande wake vitendea kazi vimekuwa vichache ikiwemo dodoso
refu
kwani mpaka kufikia Agosti 27 yalikuwa yamekwisha.
Alisema
kuwa kama vifaa hivyo havitoweza kupatika kwa haraka itafika wakati
zoezi hilo
likasimama kwa muda hadi vifaa hivyo vitakapoingia na muda
waliopewa wa zoezi la sensa ni siku saba tu na hadi kufikia agosti 28 ni
siku ya tatu vifaa hivyo vimeisha.
Aidha
aliongeza kuwa kumekuwepo kwa changamoto mbalimbali ikiwemo baadhi
ya makarani kudai kutaka kuongezewa posho kwani posho walizopewa
hazilindani na
kazi wanazozifanya zimekuwa ngumu hali inayowapelekea kufanya kazi hadi
usiku.
Pia
alisema kuwa kufuatia hayo alidai kuwa amefuatilia hadi kwa mratibu wa
sensa
mkoa huo, Bwana Juma Shabani ambapo alidai kuwa vifaa hivyo vipo njiani
na
vitawasili wakati wowote,hata hivyo alimuomba Mkuu wa Wilaya ya
Babati,Bw,Khalidi Mandia kufuatilia ili wahusika waweze kuharakisha
kufika kwa
vifaa hivyo.
Kwa
upande wake Mratibu Msaidizi wa Sensa wa Halmashauri ya Wilaya ya
Babati,Bw.Selemani Shanti alibainisha kuwa huenda siku saba walizopewa
kwa ajili ya zoezi hilo likaisha bila ya kufanikiwa kwani tatizo
lililojitokeza
kwa Halmashauri ya mji ndilo lililopo katika Halamashauri yake.
Alieleza
kuwa licha kuwepo kwa upungufu wa madodoso,pia kumekuwepo na changamoto
ya watendaji wa kata na vijiji kujichukulia mamlaka yao wenyewe ya
kuwateua
watu wanaowafahamu kwa ajili ya kuwaongoza makarani kwenye kaya kwa
lengo la
kupata posho huku wakiwasahau wenyeviti wa vitongoji ambao ndio
wanaofahamika.
Naye
Mkuu wa Wilaya ya Babati Khalidi Mandia ambaye ndiyo mwenyekiti wa
Kamati
ya Sensa amewataka waratibu hao kuhakikisha wanafuatilia kwa haraka
vitendea kazi vilivyopungua ili kuepushia gharama zingine Serikali kwa
siku
zitakazoongezwa.Hata
hivyo alisema licha ya kuwepo kwa changamoto hizo lakini hakuna tatizo
lolote
lililojitokeza la watu kugoma kuhesabiwa kama ilivyo kwa mikoa mingine
na
wilaya zake
