SERIKALI YASHAURIWA KUTUMIA RASILIMALI ZA NDANI VIZURI IKIWEMO MADINI

VIONGOZI wa Kanisa Katoliki jimbo la Musoma katika Parokia za Ingiri wilayani Rorya na Nyamwaga wilayani Tarime mkoani Mara,wameishauri serikali kutumia raslmali za ndani yakiwemo madini katika kuongeza mapato ya nchi badala ya kutegemea misaada ya wahisani.
Wamesema hatua hiyo italiwezesha taifa kuwa na mapato yake ya uhakika ambayo yatachangia kwa kiasi kikubwa kuharakisha maendeleo ya wananchi katika utekelezaji wa miradi  mingi ya maendeleo.
Wakizungumza katika ibada maalum ya mavuno katika kuelekea Jubilii ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa parokia ya Ingiri,viongozi hao wa kanisa Katoliki,wamesema kuwa hata Baba wa taifa hayati Mwalimu Julius Nyerere katika uhai wake alisimamia na  kulinda raslimali za nchi kwaajili ya watanzania ingawa hivi sasa hali ni tofauti kutokana na raslimali hizo kutowanufaisha wananchi.
                          
Naye mgeni rasmi katika ibada hiyo maalum,mbunge wa jimbo la Musoma mjini Mh Vicent Nyerere,ametumia nafasi hiyo kuwaambia waumini wa kanisa hilo, kuwa pamoja na nia njema ya serikali ya kukubali kuanzisha mchakato kuandikwa kwa katiba mpya,lakini kuna hatari kwa kupatikana kwa katiba ambayo haitakidhi mahitaji ya watanzania kutokana na wananchi walio wengi kushindwa kujitokeza kutoa maoni mbele ya tume ambayo imeundwa na rais.
         
Katika ibada hiyo ambayo imewezesha kupatikana kwa magunia 11 ya nafaka na ndoo sita za rangi,viongozi wa kanisa hilo wametumia misa hiyo kusisitiza  somo la uwajibikaji na kufanya kazi kwa bidii kama njia moja wapo ya kupambana na umasikini.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo