SERIKALI KUVIPATIA VIJIJI VYA IRAMBA UMEME WA GRIDI


SINGIDA

Serikali imeahidi kuvipatia umeme wa grid vijiji 21 vya jimbo la Iramba Magharibi na Iramba Mashariki ili pamoja na mambo mengine kuharakisha upatikaji wa maendeleo endelevu.

Akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kaselya jimbo la Iramba Magharibi Naibu Waziri wa Nishati na Madini George Simbachawene, amesema kati ya vijiji hivyo, kijiji cha Msingi na Milade, ni vya jimbo la Iramba Mashariki na vilivyobaki 19 ni vya jimbo la Iramba Magharibi.

Simbachawene ametaja baadhi ya vijiji vya jimbo la Iramba Magharibi vitakavyonufaika na mradi huo kuwa ni Kaselya, Mbelekese, Ndulungu, Malendi, Kitusha, Lugwala, Moto moto, Kizaga, Kitukuntu, Kibigiri, New Kiomboi, Makunda na Maluga.

Naibu Waziri huyo amesema vijiji hivyo vitapata umeme kwa awamu tofauti, lakini vijiji vya Mbelekese, Kaselya na Ndulungu, vitapata umeme katika mwaka huu wa fedha utakaoishia juni mwakani.

Amesema kutokana na hatua hiyo, hivi sasa hakuna haja ya vijana kukimbilia mijini ambako hakuna kazi za kufanya.

Naye mbunge wa jimbo la Iramba Magharibi Mwigulu Lameck Nchemba, amewataka wakazi wa maeneo yatakayopatiwa umeme, kutoa ushirikiano wa kutosha kwa makandarasi watakaopewa kazi ya kusambaza umeme vijijini ili kazi hiyo iweze kukamilika kwa haraka.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo