RAIS
Jakaya Kikwete hii leo amezindua awamu ya tatu ya Mfuko wa Maendeleo
ya Jamii
(Tasaf), ambayo inalenga kutoa fedha moja kwa moja kwa kaya maskini
nchini ili
ziweze kujikwamua kiuchumi.
Awali
mfuko huo ulikuwa ukitoa fedha kwa miradi mbalimbali ya jamii kama
ujenzi wa
shule, vituo vya afya, nyumba za walimu, ujenzi wa madaraja na miradi ya
watu
wenye mahitaji maalumu kama walemavu na watu wanaoishi na virusi
vinavyosababisha ugonjwa wa ukimwi.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Tasaf, Ladislaus Mwamanga alisema jijini Dar es Salaam kuwa uzinduzi huo umefanyika mjini Dodoma.
“Awamu
ya pili imekuwa na mafanikio makubwa… Madhumuni ya awamu ya tatu ni
kuendeleza
mafanikio yaliyopatikana awamu ya pili ili kuwezesha kaya maskini
kuongeza kipato na fursa za kuinua kiwango cha matumizi yao.” alisema
Mwamanga.
Alisema
awamu hii itaendeshwa kwa kipindi cha miaka 10 na itakuwa na awamu mbili
za
miaka mitano mitano.
Ili
kufanikisha mpango huo, alisema hadi jana, wafandhili pamoja na
Serikali,
walikuwa wamechangia Dola za Marekani 272.9 milioni karibu na Sh 436.64
bilioni.
Alisema
fedha hizo zitatumika kwenye kipindi cha miaka mitano ya kwanza ya awamu
hiyo.
Mtindo
wa Tasaf kuzisaidia familia masikini moja kwa moja, alisema ulitokana na
mradi
wa majaribio uliofanyika wakati wa utekelezaji wa awamu ya pili na
kuonyesha
utaweza kuondoa umasikini unaozikumba kaya nyingi nchini.
Mkakati
huo aliuelezea utasaidia kaya hizo kutatua matatizo mbalimbali kama vile
elimu,
afya na maji na utawalenga wazee, watoto na miradi ya kuongeza kipato
kwa wenye
uwezo wa kufanya kazi.
Akizungumzia
uzinduzi huo, Mwamanga alisema baadhi ya kaya masikini zilizofaidika
katika
mradi wa majaribio watatoa ushuhuda.
Vile
vile akasema “hafla hiyo itatoa fursa kwa Serikali kuweka bayana dhamira
yake
ya kupanua na kuwafikia wananchi wengi zaidi” kwenye mpango wa
kukabiliana na
uamsikini.
Akizungumzia
awamu ya pili ya Tasaf, Mwamanga alisema pamoja na kuonyesha mafanikio,
changamoto kubwa ilikuwa ni uwezo mdogo wa kifedha wa kutekeleza miradi
yote
iliyobuniwa na wananchi.
“Miradi
iliyopangwa kutekelezwa ilikuwa 5,950 (sawa na asilimia 10) wakati
maombi
kutoka kwa wananchi yalifikia 102,275,” alisema Mwamanga.
Akizungumzia
juu ya namna kaya masikini zitakavyopatikana katika awamu ya tatu,
Mtaalamu wa
Utafiti na Ushirikishwaji wa Mambo ya Kijamii wa Tasaf, Amedeus
Kamagenge
alisema watatumia mikutano mikuu ya kijiji na mitaa.
Vile
vile vigezo sahihi, akaeleza kuwa vitatambuliwa baada ya sifa za
wahusika
kuchambuliwa na kompyuta zenye programu maalumu za kuchambua mifumo ya
umasikini.
