MWANAMKE AKUTWA AMEUAWA NA WATU WASIOJULIKANA


MWANAMKE  mmoja mkazi wa Kilototoni wilayani Moshi Vijiji amekutwa ameuwawa na watu wasio julikana nje ya nyumba yake aliyo kuwa akiishi na kumjeruhi vibaya kichwani.

Kaimu kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro Koka  Moita, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo alisema majira ya saa 01:35 usiku Agusti 16 mwaka huu katika eneo la Kilototoni Wilayani Moshi Vijijini kulitolewa taarifa katika kituo cha Polisi Himo kwamba kunamfanya biashara moja amekutwa ameuwaa nje ya Nyumba yake.

Alisema baada ya askari kupokea taarifa hizo walikwenda hadi eneo la tuko na kuukuta mwili wa marehemu Monica John (59) ukiwa pembeni kidogo na nyumba yake  na kwamba uchunguzi waawali unaonyesha kuwa marehemu huyo ameuwawa kwa kipigo kikali  kutokana na kukutwa na majeraha sehemu za kichwani.

Kufuati tukio hilo la mauaji jeshi la polisi mkoani humo limetoa wito kwa wananchi  kuwa makini na watu wasio wafahamu katika maeneo yao na kwamba endepo watabaini kuwepo kwa hali tofauti watoe taarifa polisi kwaajili ya ulinzi zaidi.

Moita alisema matukio ya mauaji yamekuwa yakitokea mara kwa mara kutokana na uzembe wa wananchi kuto kutoa taarifa polisi mara wabainipo kuwa na hali isiyo kuwa ya kawaida katika maeneo yao

Aidha ajeshi la polisi mkoani hapa limemshikilia mume wa marehemu kwa mahoojiana zaidi kuhusiana na tukio hilo la mauaji  na kwamba mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hosptali ya mkoa ya Mawenzi kwa uchunguzi zaidi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo