MKUU WA WILAYA YA MAKETE AWA WA KWANZA KUHESABIWA KATIKA SENSA WILAYANI MAKETE, ATOA WITO KWA WANAMAKETE


Ikiwa usiku wa kuamkia hii leo zoezi la sensa ya watu na makazi limeanza kutekelezwa nchi nzima, wilayani Makete zoezi hilo limeanza kwa amani na utulivu kama ilivyotarajiwa huku mkuu wa wilaya hiyo akiwa wa kwanza kuhesabiwa

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuhesabiwa, mkuu wa wilaya ya Makete ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya sensa wilaya Bi Josephine Matiro amewataka wananachi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa makarani wa sensa

Amesema maswali yanayoulizwa ni mepesi na yanayojibika hivyo haoni sababu ya wananchi wake kuogopa kuzungumza ama kutoa taarifa kwani kila kitu kipo wazi na haichukui muda mrefu

“Unajua watu wengi wanakuwa na hofu, mimi naona hizo hofu hazina maana kwanza maswali yenyewe ni marahisi, hayaumizi kichwa na wala hayapotezi muda, cha masingi makarani wa sensa wakifika kwako wewe kama mkuu wa kaya ni kutoa taarifa tuu, kama nlivyofanya mimi kwa kuwa nami nimeshahesabiwa muda mchache uliopita na namshukuru Mungu kuwa wa kwanza hii leo kuhesabiwa”alisema

Amesema zoezi la sensa ya watu na makazi haliathiri utendaji kazi wa shughuli za wananchi na kuwataka wananchi kutoacha kufanya shughuli zao kutokana na kusubiri kuhesabiwa

Pia ameitaka jamii kusaidia kuonesha maeneo tete ambayo watu huwepo ikiwemo waliopo misituni kupasua mbao, ama waliopo maporini kuchoma tofali, ili makarani wa sensa wawafuate huko waliko na taarifa zao ziweze kuchukuliwa na makarani wa sensa

Matiro amewataka wakuu wa kaya kutayarisha ipasavyo taarifa za watu wote waliolala kwenye kaya yake usiku wa kuamkia leo, ili aweze kuzitoa kwa makarani wa sensa pindi watakapofika kwenye kaya zao kuendesha zoezi la sensa

Zoezi la sensa ya watu na makazi linaendelea kutekelezwa nchi nzima likiongozwa na kauli mbiu isemayo SENSA KWA MAENDELEO JIANDAE KUHESABIWA na litaendeshwa kwa siku saba mfululizo hivyo wananchi mnaombwa kutoa ushirikiano


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo