KAMATI YA SENSA WILAYA YA MAKETE YAENDELEA KUHAMASISHA KUHUSU SENSA

 Mwenyekiti wa kamati ya sensa na mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro
 Mjumbe wa kamati ya sensa wilaya na Katibu wa CCM wilaya ya Makete Miraji Mtaturu
                                   Washiriki wakisikiliza kwa makini

Viongozi wa dini, walemavu na wamiliki wa nyumba za kulala wageni wilayani Makete wametakiwa kutoa ushirikiano wa kutosha ili kufanikisha zoezi la sensa ya watu na makazi wilayani humo

Hayo yamebainika wakati kamati ya sensa wilaya ya Makete chini ya mwenyekiti wake ilipokutana na makundi hayo kwa lengo la kuwapatia elimu ya sensa ili nao wakapeleke elimu hiyo kwa jamii

Akiungumza na makundi hayo mjumbe wa kamati ya sensa ambaye pia ni katibu wa CCM wilaya ya Makete Bw. Miraji Mtaturu amesema viongozi wa dini wao wana nafasi kubwa ya kuonana na waumini wao hivyo amewaomba kufikisha elimu hiyo kwa waumini wao

“unajua ndugu zangu viongozi wa dini ni kundi linaloaminika kwa jamii, tunawaombeni elimu hii tuliyowapa mkaifikishe kwa jamii, maana serikali inafanya kazi na kila mtu ikiwemo ninyi, siku zimebaki chache naomba tusaidiane tafadhali”alisema Mtaturu

Amesema sensa ya watu na makazi itaisaidia serikali kutambua idadi ya watu nchini pamoja na mambo mengine ambayo yatasaidia serikali kuboresha huduma zake na maendeleo katika sekta mbalimbali hapa nchini

Kwa upande wake Bw. Edwin Moshi ambaye naye ni mjumbe wa kamati ya sensa wilaya ameelezea umuhimu wa wakuu wa kaya kutoa taarifa sahihi kwa makarani wa sensa na si kutoa taarifa za kubuni pamoja na kuhakikisha kila mtu aliyelala kwenye kaya yake ahesabiwa

Ameongeza kuwa ni muhimu kwa kila mtu kuhesabiwa mara moja tu wakiwemo watoto wachanga na walemavu kwani wengi wao wamekuwa wakisahaulika kuhesabiwa kutokana na dhana potofu iliyopo kwa jamii kuwa hawahusiki, na kuongeza kuwa taarifa zitakazokusanya zitakuwa za siri na zitatumika kwa malengo yaliyokusudiwa

Amewatoa hofu wananchi kuwa taarifa hizo zitatumika kwa ajili ya freemasons, kujua utajiri wa watu ili wafilisiwe pamoja na kuwahamisha wananchi kwenye maeneo yao, hivyo wnanchi wasiwe na hofu, taarifa hizo zitatumika kwa ajili ya maendeleo ya nchi

Akihitimisha mwenyekiti wa kamati ya sensa wilaya ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Makete Mh. Josephine Matiro amewaambia waalikwa hao kuwa wao ni wadau wazuri katika kufanikisha zoezi la sensa wilayani humo huku akiwataka wamiliki wa nyumba za kulala wageni kutoa elimu kwa wahudumu wao na kutambua kuwa usiku wa kuamkia Agosti 26 wawaambie wageni wao kuwa wajiandae kuhesabiwa usiku huo

Ameongeza kwamba Agosti 25 kuamkia Agosti 26 sensa itafanyika katika makundi tete ikiwemo kwenye nyumba za kulala wageni kwa kuwa wageni hao wengi wao asubuhi hawapatikani, na makarani watakaotekeleza` zoezi hilo watakuwa na vitambulisho maalum

Zoezi la uhamasishaji wananchi kushiriki sensa ya watu na Makete usiku wa kuamkia Agosti 26 linaendelea wilayani Makete ambapo tayari uhamasishaji umefanyika hii leo katika kata za Tandala, Iwawa, Bulongwa na Matamba zoezi linaloongozwa na kamati ya sensa wilaya ya Makete na linaendelea wilaya nzima


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo