MAMLAKA ZA MAGEREZA AFRIKA MASHARIKI ZATAKIWA KUBADILISHANA UZOEFU KATIKA USIMAMIZI WA ADHABU

 Arusha, 
 
Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uganda Hillary Onek ameshauri Mamlaka za Magereza Afrika Mashariki (EAC) kubadilishana uzoefu na desturi zilizo njema katika usimamizi wa adhabu za vifungo kwa wafungwa.
‘’Tunatakiwa kuhakikisha kwamba magereza yetu ya kikoloni yanaangalia utu na haki kwa wafungwa kama maadili yake muhimu,”alieleza waziri wakati akiuuhutubia mkutano wa siku tatu wa wakuu wa Magereza na Vyuo vya Mafunzo mjini Kampala ambao ulimalizika juzi, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Sekretarieti ya EAC.
Alisema kuwa nchi za Afrika Mashariki zinatakiwa kuweka msisitizo kwenye maboresho katika magereza ili kuwawezesha wafungwa wanapomaliza vifungo vyao kujengeka na kuwa werevu.
‘’Tunauwezo na lazima tusiruhusu wafungwa waliobadika kuwa wazalishaji wa wahalifu sugu katika jamii mara wanapoachiwa kutoka gerezani,” alisisitiza.
Alisema nchi za Afrika Mashariki ziepuke ukoloni katika magereza ambapo Waafrika walikuwa wanadhalilishwa utu wao.
“Magereza yetu baada ya uhuru lazima yawe na sura ya utu, utaalam na yatoe malengo yaliyo kusudiwa,” Waziri Mganda alifafanua, na kuongeza kuwa magereza yasiwe mahali pa mapigano, kufungiwa na kutendewa unyama kwa wafungwa.
Naibu Katibu Mkuu wa EAC, anayeshughulikia Shirikisho la Kisiasa, Dk.Julius Rotich, alisema magereza na vyuo vya mafunzo vimejumuishwa katika mipango ya ulinzi na usalama katika kanda kwa nchi wanachama wa EAC.
Dk.Rotich alisema hii ilikuwa muhimu kwa EAC, akisema itachangia katika kufanikisha utekelezaji wa utaratibu wa soko la pamoja, hatua ya pili ya mwingiliano wa kikanda.
Hatua ya kwanza ya mtangamano ilikuwa Umoja wa Forodha ambayo ilianza kutumika Januari 2005. Nchi wanachama sasa yanajadiliana kufikia Umoja wa Sarafu.
Hata hivyo, Naibu Katibu Mkuu huyo alibainisha kuwa sekta ya Ulinzi na Usalama bado inakabiliwa na changamoto katika ufadhili.
‘’Hii haina matumaini mazuri katika mtangamano imara. Wakati Sekretarieti ya EAC na nchi wanachama zikijaribu kutafuta njia mbadala za ufadhili wa shughuli za kikanda, mamlaka za Magereza zitatakiwa kila mara kuunga mkono mikakati iliyopangwa,” alisema ofisa huyo wa EAC.
Mwanyekiti wa Mkutano, Daniel Mutua, kutoka Kenya, alisititiza huduma za kisasa na zinazofaa kwenye magereza katika kanda ili kutimiza malengo ya mtangamano wa EAC.
‘’Mafunzo na uandaaji bora wa mamlaka katika magereza utawezesha kutoa matunda yaliyokusudiwa,” aliseama. Wajumbe pia walitembelea magereza mjini Kampala.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo