MAMLAKA YA MJI TARIME YAKUSANYA ZAIDI YA MILIONI 220


Tarime.
 
MAMLAKA ya Mji Mdogo wa Tarime kupitia vyanzo vyake vya ndani vya mapato imekusanya jumla ya 220,788,095.97 sawa na asilimia 85% ya kiasi kilichokuwa kimekasimiwa kipindi cha mwaka wa fedha ulioishia tarehe 30 mwezi juni  2012.
 
Hayo yalibainishwa na Mwenyekiti wa mamlaka ya mji mdogo wa Tarime Christoper Mantago wakati wa kikao cha wajumbe wa baraza la mamlaka ya mji huo,Mantago alisema kuwa  kwa kipindi hicho mamlaka ya mji ilikisia kutumia jumla ya 260,026,600 na kiasi halisi kilichotumika ni 212,811,995.95 sawa na asilimia 82 ya matumizi yaliyokasimiwa.
 
Pia Mantago alisema kuwa katika  upande wa usafi wa mazingira mamlaka hiyo imefanikiwa kushika nafasi ya sita Kitaifa na kwamba malengo yao ni kushika nafasi ya kwanza.
 
Mantago alisema kuwa pamoja  na juhudi hizo za mamlaka katika makusanyo bado mamlaka hiyo inakabiliwa na tatizo la kutokuwa na baadhi ya wataalamu wanaohitajika hususani mwanasheria na muhandisi wa ujenzi.
 
Aliongeza kuwa baadhi ya wafanya biashara wanaotumia vibanda vilivyoko soko kuu na stendi ya mabasi kwa kutokuafikiwa kusaini mkataba utakao wawezesha kulipa mamlaka ya mji kodi ya vibanda.
 
Mkuu wa Wilaya ya Tarime John Henjewele aliipongeza mamlaka hiyo kwa makusanyo mazuri ya mapato kupitia vyanzo vyake vya ndani ambapo aliwataka kuzidi kuongeza zaidi makusanyo huku akisisitiza siasa isihusishwe katika maendeleo ndani ya mamlaka ya mji mdogo wa Tarime kwani inakwamisha maendeleo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo