Moshi
MKURUGENZI wa manispaa ya moshi mkoani Kilimanjaro, Bernadette Kinabo amewataka madereva wanaoingiza magari yao katika stendi kuu ya mabasi moshi kulipa ushuru ulioongezeka na kuacha kulumbana kwa kuwa kiwango kilichoongezwa hakita badilishwa.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana kuhusiana na
madereva wanaoingiza magari katika stendi na kukataa kulipa ushuru kwa madai kuwa ushuru huo umeongezwa bila kushirikisha madereva hao, Kinabo alisema kiwango hicho hakitabadilishwa na wanatakiwa kulipa ili manispaa iweze kujenga barabara zote kwa kiwango cha lami.
Kinabo alisema madereva hao wanakataa kulipa kutokana na wakala
aliyepewa tenda ya kukusanya ushuru ndani ya manispaa hiyo kushindwa
kusimamia zaezi la kupanga magari na kukusanya ushuru huo
“tumeongeza ushuru kutoka shilingi 500 hadi 1500 kwa mabasi madogo na shilingi 1000 hadi 2000 kwa mabasi makubwa yanayokwenda mikoani , kwa sababu tumekaa muda mrefu sana bila kuongeza ushuru takribani miaka kumi sasa”alisema kinabo.
Mkurugenzi huyo alisema zoezi hilo limekwama kutokana na wakala
aliyepewa tenda hiyo kushindwa kupanga magari na kutoza ongezeko hilo na kwamba manispaa inaweka wakala mwingine ambaye ataweza kusimamia zoezi la kutoza vingo vya ushuru vilivyoongezeka.
Nao baadhi ya madereva hao ambao ni Daniel Kimwaga, Muhamed bonge na Mwidoe Rajabu walisema hawatalipa kiwango hicho na badala yake
watalipa kiwango cha zamani ambacho walichokubalina na manispaa hiyo
kutokana na manispaa kutowashirikisha madereva hao kuhusiana na
mabadiliko ya ushuru huo.
Walisema hawatolipa kwa sababu hakuna babadiliko yoyote yaliyofanywa
tangu waanze kulipa ushuru huo na kwamba mabasi mengine hayana sehemu ya kuegesha bali wanaegesha pembezoni mwa barabara.
Madereva hao walisema ni muda wa mwezi mmoja na nusu sasa tangu waache kulipa ushuru kutokana na manispaa kuongeza ushuru huo kupita kiasi na kutofanya mabadiliko yoyote katika stendi hiyo.
MKURUGENZI wa manispaa ya moshi mkoani Kilimanjaro, Bernadette Kinabo amewataka madereva wanaoingiza magari yao katika stendi kuu ya mabasi moshi kulipa ushuru ulioongezeka na kuacha kulumbana kwa kuwa kiwango kilichoongezwa hakita badilishwa.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana kuhusiana na
madereva wanaoingiza magari katika stendi na kukataa kulipa ushuru kwa madai kuwa ushuru huo umeongezwa bila kushirikisha madereva hao, Kinabo alisema kiwango hicho hakitabadilishwa na wanatakiwa kulipa ili manispaa iweze kujenga barabara zote kwa kiwango cha lami.
Kinabo alisema madereva hao wanakataa kulipa kutokana na wakala
aliyepewa tenda ya kukusanya ushuru ndani ya manispaa hiyo kushindwa
kusimamia zaezi la kupanga magari na kukusanya ushuru huo
“tumeongeza ushuru kutoka shilingi 500 hadi 1500 kwa mabasi madogo na shilingi 1000 hadi 2000 kwa mabasi makubwa yanayokwenda mikoani , kwa sababu tumekaa muda mrefu sana bila kuongeza ushuru takribani miaka kumi sasa”alisema kinabo.
Mkurugenzi huyo alisema zoezi hilo limekwama kutokana na wakala
aliyepewa tenda hiyo kushindwa kupanga magari na kutoza ongezeko hilo na kwamba manispaa inaweka wakala mwingine ambaye ataweza kusimamia zoezi la kutoza vingo vya ushuru vilivyoongezeka.
Nao baadhi ya madereva hao ambao ni Daniel Kimwaga, Muhamed bonge na Mwidoe Rajabu walisema hawatalipa kiwango hicho na badala yake
watalipa kiwango cha zamani ambacho walichokubalina na manispaa hiyo
kutokana na manispaa kutowashirikisha madereva hao kuhusiana na
mabadiliko ya ushuru huo.
Walisema hawatolipa kwa sababu hakuna babadiliko yoyote yaliyofanywa
tangu waanze kulipa ushuru huo na kwamba mabasi mengine hayana sehemu ya kuegesha bali wanaegesha pembezoni mwa barabara.
Madereva hao walisema ni muda wa mwezi mmoja na nusu sasa tangu waache kulipa ushuru kutokana na manispaa kuongeza ushuru huo kupita kiasi na kutofanya mabadiliko yoyote katika stendi hiyo.
