MANYARA.
Imebainishwa
kuwa ili kupambana na
uhalifu jeshi la polisi mkoani Manyara linafanya msako na kuimarisha
doria
katika maeneo mbalimbali ndani ya mkoa wa manyaya.
Hayo
yamebainishwa na kamanda polisi
mkoa wa Manyara Akili Mpwapwa wakati alipokuwa akiongea na wandishi wa
habari
mkoani hapa.
Alibainisha kuwa
katika msako
huo watuhumiwa wa makosa mbalimbali wamekamatwa kwakukuhusika na matukio
ya
uhalifu kama vile kupatikana na kwa Bhangi,mirungi na makosa ya usalama
barabarani pamoja na pombe aina ya moshi gongo.
Kamanda Mpwapwa
alisema kuwa katika
kupatikana na silaha na risasi bila kibali katika barabara kuu itokayo
Arusha Babati walikamatwa watuhumiwa wawili Salimu Mohamed na Paulo Issa
wakiwa
na bunduki moja aina ya rifle 458 no 59477,risasi sita,maganda mawili na
risasi
nyingine ndogo mbili ambazo hazijafahamika ni za bunduki gain.
Aliendelea
kusema kuwa watuhumiwa
hao walipohojiwa walikiri kuwa wao ni majangili na walikuwa safarini
kwenda
kuwinda Tembo katika hifadhi ya Tarangire kupitia Galapo,watuhumiwa wote
wamefikishwa mahakamani.
Alisema kuwa
huko maeneo ya Mdori
Hamisi Gidamrisi Giau alikamatwa na bunduki rifle 458 no 987660 ambayo
nayo
alikiri inatumika na ujangiri naye amefikishwa mahakamani.
‘’Jamani
waandishi wa habari kiasi
cha 27 kg za Baghi zilikamatwa sehemu mbalimbali za mkoani hapa pia
katika
msako huo watuhumiwa sita walikamatwa kwa makosa ya kupatikana kwa
Baghi
na kiasi cha mirungi 160 kg zilikamatwa katika msako watuhumiwa watatu
walikamatwa watuhumiwa wote wamefikishwa mahakamani.’’Alisema Kamanda
Mpwapwa.
Aliongeza kuwa
kutokana na
msako uliofanywa maeneo mbalimbali ya mkoa wa Manyara kiasi cha lita
1713 za
pombe haramu ya moshi(gongo) zilikamatwa,jumla ya watuhimiwa 82
walikamatwa na
kufikishwa mahakamani,kati yao 62 walipatikana na hatia,wengine 20 kesi
zao zinaendelea na mitambo sita ya kutengenezea gongo ilikamatwa katika
misako hiyo.
Kamanda Mpwapwa
alisema kuwa kwa
upande wa udhibiti wa makosa ya uaslama Barabarani jumla ya makosa
yaliyokamatwa ni 519,makosa ya ubovu wa vyombo vya usafiri ni 85,makosa
mengineyo ni 434 ambapo jumla ya shilingi milioni 15,570,000
zilikusanywa
kutokana na faini ya papo kwa hapo.
Alisisitiza
kuwa jeshi la polisi
mkoani hapa limefanikiwa kwa zoezi zima la msako na kudhibiti makosa ya
usalama
barabarani katika kipindi cha mwezi julai 2012 kutokana na mahusiano
mazuri
baina ya jeshi hilo na raia wema ambao wamewezesha kwa njia moja au
nyingine
kutoa taarifa zilizoleta mafanikio katika chombo chao cha jeshi hilo kwa
kuzingatia sera ya jeshi la polisi Tanzania kuimarisha ulinzi shirikishi
na
polisi jamii.
Ametoa wito kwa
wananchi wa mkoani
hapa kuondoa wasiwasi na kutoa taarifa katika chombo chao cha jeshi la
polisi
ili kuweza kufanikisha kukamata na kuzuia au kupunguza uhalifu ndani ya
mkoa
huo na kwamba siri zao zinatunzwa.
Pia alimalizia
kwa kuwaonya wananchi
ambao wanaojihusisha na vitendo vya uharifu kama vile unyang’anyi wa
kutumia
nguvu,kupatikana na baghi,mirungi na makosa ya usalama barabarani kuacha
vitendo hivyo mara moja ambapo jeshi hilo limejipanga vizuri kupambana
na
uhalifu wa aina yoyote wale wataendelea kujihusisha na vitendo vya
uhalifu
watakamatwa na kufikishwa mahakami ili sheria ichukue mkondo wake dhidi
yao .
