Akizungumza
na wanahabari sokoni hapo katibu wa soko hilo Bw. Asifiwe Luvanda amesema
kufuatia mkutano walioufanya na mkurugenzi Agosti 17 mwaka huu, waliagizwa
kutengeneza mara moja choo hicho kwani kimejaa, hivyo wameanza kutekeleza agizo
hilo
Amesema
hatua ambayo wameichukua hadi sasa ni kupeleka taarifa hizo kwa Bwana Afya wa
wilaya Boniphace Sanga kuona kama watatakiwa
kutengeneza choo kipya ama kuna namna ambayo itaweza kutumiwa, ili choo hicho
kiendelee kutumika
Amesema
ushirikiano ndio unahitajika zaidi kutoka kwa wafanyabiashara wote, idara ya
afya wilaya ya Makete pamoja na wadau mbalimbali ili kutatua kero hiyo
“Unajua
mimi nina wasiwasi sana kama tutafanikiwa katika
hili ingawa sisi kama viongozi inabidi
tutekeleze agizo la mkurugenzi, lakini nina wasiwasi na ushirikiano kutoka kwa
wafanyabiashara wenzangu”alisema Luvanda
Waandishi
wa habari waliofika eneo hilo wameshuhudia choo
hicho kikiwa kimejaa na pia ipo hatari ya kutokea mlipuko wa magonjwa kama vile kipindupindu muda wowote kuanzia sasa kwa kuwa
bado wafanyabiashara hao wanaendelea kujisaidia katika choo hicho ingawa
kimejaa
Hadi
mwandishi wetu anaandika habari hii juhudi za kumpata bwana afya wilaya ya
Makete Boniphace Sanga kuhakikisha kama
taarifa hizo zimeshafikishwa ofisini kwake zimegonga mwamba mara baada ya simu
yake kutopatikana
Agosti
17 mwaka huu mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya makete alifanya
mkutano na wafanyabiashara hao ambapo pamoja na mambo mengine aliwaagiza
viongozi hao kutatua kero ya choo ambacho kimejaa