DC MAKETE MH. JOSEPHINE MATIRO AKIFUNGUA MAFUNZO HAYO
MRATIBU WA SENSA MAKETE BI NURU MWENDAPOLE AKIZUNGUMZA NA WASHIRIKI
DODOSO REFU LA SENSA 2012
Na Edwin Moshi, Makete
Makarani na wasimamizi wa sensa ya watu na makazi wilayani
Makete wametakiwa kuhakikisha wanatekeleza zoezi hilo
kwa umakini kama serikali ilivyowaagiza ili malengo ya zoezi hilo yafanikiwe
Akifungua mafunzo kwa makarani na wasimamizi hao wa sensa
wilayani Makete hii leo, Mwenekiti wa kamati ya sensa wilayaya ya Makete ambaye
pia ni mkuu wa wilaya hiyo Mh. Josephine Matiro amesema dhamana waliyopewa ni
kubwa na itatekelezwa na wao katika wilaya hiyo hivyo wanatakiwa kufuata
mafunzo wanayopatiwa kwani ni njia pekee ya kufanikisha zoezi hilo
Amesema pamoja na mambo mengine wanamafunzo hao wanatakiwa
kutunza usiri mkubwa wa taarifa za sensa ambazo watazikusanya kwa watu pamoja
na kuuliza maswali kadri ya uwezo wao ili waweze kuelewa namna watakavyokwenda
kutekeleza zoezi hilo
Mh. Matiro ameeleza pia mandalizi ya sensa kwa wilaya ya
Makete yamekamilika na mengine yanaendelea kutekelezwa kwani maandalisi mengine
yanahitaji utekelezaji wake kwa jinsi siku zinavyozidi kwenda
“Ndugu zangu naomba niwatoe hofu, serikali ipo makini na
maandalizi hapa wilayani yamekamilika hivyo tunaomba msituangushe, mmepewa
dhamana kubwa ya kutekeleza zoezi la sensa ngazi ya wilaya, mpo waalimu tena
ambao mnaaminika kuliko watu wengine, lakini pia na wote mliochaguliwa kufanya
zoezi hili nawaombeni mlifanikishe ipasavyo” alisema Matiro
Ameongeza kuwa kazi ya uhamasishaji ngazi ya wilaya
inaendelea kwa kutumia rasilimali mbalimbali zilizopo wilayani hapo, ikiwemo
redio, matangazo kwa uma, mikutano ya hadhara, makanisani, misikitini, mabango
na vipeperushi mbalimbali, hivyo wananchi wengi wanauelewa wa kutosha kuhusu
sensa
Awali akimkaribisha mkuu wa wilaya, mratibu wa sensa ngazi
ya wilaya Bi. Nuru Mwendapole amesema jumla ya washiriki 484 wilaya nzima
wanapatiwa mafunzo hayo wakiwemo wadadisi wa dodoso refu wapatao 430,
wasimamizi 32 pamoja na wadadisi wa ziada wapatao 22, na wote hao wanapatiwa
mafunzo katika vituo vine tofauti ambavyo ni Iwawa, Tandala, Bulongwa na
Matamba
Mkuu huyo wa wilaya pamoja na wajumbe wa kamati ya sensa
wilaya mbali na kushiriki katika ufunguzi wa mafunzo hayo pia walishiriki
wakati wa mafunzo na kujionea jinsi washiriki walivyokuwa wakipatiwa mafunzo ya
utekelezaji wa zoezi la sensa linalotarajiwa kufanyika usiku wa kuamkia Agosti
26 mwaka huu


