MARA IMEJIPANGA KUKAMILISHA ZOEZI LA SENSA KAMA ILIVYOPANGWA

MUSOMA
 
MKOA wa Mara umekamilisha tayari umechukua hatua za haraka za kuhakikisha zoezi la Sensa ya watu na makazi linafanikiwa kama lilivyopangwa katika visiwa 30 ambavyo vimo ndani ya ziwa Victoria.
 
Mratibu wa Sensa mkoa wa Mara Bw Ramadhan Mbega,amesema mbali na kuyabainisha maeneo hayo pia imetenga maeneo ya kuhesabia watu katika maeneo ya hifadhi za taifa ya Serengeti na mapoli ya akiba yanayopakana na hifadhi hiyo.
 
Hata hivyo Bw Mbega,amewataka wananchi wa mkoa wa Mara kuachana na dhana potofu ya baadhi ya watu kuwa endapo watahesabiwa katika zoezi hilo wanaweza kupoteza maisha ama kushindwa kuzaa.
 
Bw.Mbega amesema si kweli kuwa watu wanaweza kuzaa au kupoteza maisha na kuongeza kuwa zoezi hilo linalenga kuwezesha taifa kupata takwimu sahihi za watu na makazi kwaajili ya kuwahudumia vema wananchi wake.
 
Mbali na hivyo mratibu huyo amempongeza mkuu wa mkoa wa Mara Bw.John Tuppa kwa kuwa mstari mbele kuhamasisha wananchi kuhusu zoezi hilo la Sensa huku akitoa wito kwa wananchi kujitokeza katika zoezi hilo
 
Na www.mwanawaafrika.blogspot.com


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo