MAHAKAMA YAKOSA HAKIMU WA KUDUMU


BUTIAMA

Mahakama ya mwanzo ya Kukirango katika wilaya ya Butiama mkoani Mara haina hakimu wa kudumu na hivyo kusababisha kesi nyingi kuahirishwa mara kwa mara.

Wakiongea katika eneo la mahakama hiyo,baadhi ya wananchi wamesema kuwa kumekuwepo na karani mmoja katika mahakama hiyo ambaye kazi yake imekuwa kuahirisha kesi.

Wamesema kukosekana kwa hakimu wa kudumu katika Mahakama hiyo baadhi ya kesi zimekuwa zikiendeshwa kwa zaidi ya miaka miwili, huku wengine wakipeleka kesi zao katika Mahakama ya mwanzo ya mjini Musoma.

Aidha wananchi hao wamesema kuwa nyumba zilizojengwa wakati wa ukoloni kwa ajili ya hakimu na karani zimegeuka kuwa makazi ya popo na mchwa.

Mahakama ya Mwanzo ya Kukirango inahudumia wananchi wa kata nne zilizopo katika tarafa ya Makongoro ingawa kwasasa imeshindwa kutoa huduma ipasavyo kutokana na kutokuwa na hakimu wa kudumu.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo