WANAMAKETE USAFI NDIO 'DILI'

Wito umetolewa kwa wananchi wilayani Mekete  kuwa na desturi ya kufanya usafi wa mazingira wa maeneo yanayowazunguka kuanzia ngazi ya kaya

Hayo yamezungumzwa na Afisa maendeleo ya jamii wa kta ya isapulano bw, Denis Sinene wakati wa ukaguzi wa usafi wa mazingira katika kijiji cha luvulunge wilayani makete

Bw,Sinene amesema kuwa wapo wananchi wanaosubiri hadi watangaziwe kuwa kuna ukaguzi wa usafi wa ndipo wanaanza kusafisha mazingira yao hali inayosababisha milipuko ya magonjwa mbalimbali miongoni mwa jamii

Aidha amesema kwasasa watafanya ukaguzi wa usafi kimyakimya bila ya kutoa taarifa na pia kuwataka  wakazi wa maeneo hayo kujenga vyoo vya kisasa vya kutumia tofali nakuacha kutumia mabanzi katika kujenga vyoo hivyo

Na: Obeth Ngajilo & Anitha Sanga


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo