WAZIRI WA MALIASILI BALOZI KAGASHEKI AKABIDHIWA OFISI RASMI LEO

Aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Ezekieli Maige katikati  Akiongea na waandishi wa habari leo .katika. Hafla ya kukabidhi ofisi kwa waziri mpya wa wizara hiyo Mh Balozi Khamis Kagasheki ambaye ni wa kwanza kushoto na Naibu Waziri wake Mhe.Lazaro Nyarandu ambaye ni wa kwanza kulia.katika ukumbi wa mikutano wa wizara ya maliasili na utalii jijini Dar es salaam.
(PICHA NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE)
Naibu Waziri wa maliasili na utalii Mhe. Lazaro Nyarandu akisisitiza jambo katika hafla hiyo ya makabidhiano ya ofisi iliyofanyika leo katika wizara ya maliasili na utalii.
Waziri wa maliasili na utalii  Mh; Balozi Khamisi Kagasheki akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kukabidhiwa ofisi rasmi leo ambapo amesema watendaji wote walioguswa na kashfa mbalimbali katika wizara hiyo watachukuliwa hatua za kisheria mara moja iwezekanavyo.
 
 
Aliyekuwa Waziri wa maliasili na utalii Mhe.Ezekieli Maige kulia wakiingia ofisini na waziri mpya wa wizara hiyo na Naibu wake tayari  kuanza kazi rasmi baada ya kukabidhiwa ofisi leo.
Waziri wa maliasili na utalii  Mh. Balozi Khamisi Kagasheki akiwa kwenye picha ya pamoja na watendaji wa wizara hiyo.
Waziri wa maliasili na utalii  Mh. Balozi Khamisi Kagasheki akiwa kwenye picha ya pamoja na aliyekuwa waziri wa maliasili na utalii Mhe.Ezekieli Maige mara baada ya makabidhiano ya ofisi leo.
Baadhi ya waandishi wa habari walioudhuria katika hafla hiyo 
Picha kwa hisani ya fullshangwe blog


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo