WADAU TUSHIRIKIANE KUPAMBANA NA VITENDO VYA UNYANYASAJI WA KIJINSIA KWA WANAFUNZI


Viongozi wa serikali za vijiji wazazi na wadau wengine wa elimu wametakiwa kutoweka maslahi yao wenyewe katika kuwanusuru wanafunzi kuondokana na tatizo la unyanyasaji wa kijinsia mashuleni

Hayo yamesemwa na mkurugenzi wa shirika la Support makete to self support (SUMASESU) Bw. Egnatio Mtawa wakati wa uzinduzi wa mradi wa shule salama unaendeshwa na shirika hilo kwa ufadhili wa RFE

Amesema shirika la SUMASESU linajitahihidi kuhakikisha jamii ya Makete inaishi kwa usawa, amani, maendeleo pamoja na kuwa na afya nzuri na hilo litafanikiwa 

Mradi huo  wa shule salama utazihusisha shule nne za sekondari ya Itamba, Matamba, Ikuwo na Mlondwe  na mradi huu utaendelea hadi mwezi wa Februari mwaka 2013

Na: Aldo Sanga & Veronica Mtauka


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo