WANAMAKETE JIJENGEENI DESTURI YA KUHIFADHI MAZAO YA CHAKULA


Wananchi wilayani Makete wametakiwa kuweka akiba ya chakula na kuacha tabia ya kuuza mazao ya chakula pindi wanapoyavuna

Hayo yamezungumzwa na mwenyekiti wa kitongoji cha RC “A” katani Iwawa Bw. Mapambano Mahenge wakati akizungumza na wananchi waliohudhuria kwenye mkutano wa hadhara wa kitongoji hicho, na kuongeza kuwa wapo wananchi wanaouza mazao yao baada ya kuvuna bila kujiwekea akiba hali inayopelekea upungufu wa chakula miongoni mwa familia nyingi wilayani hapo

Amesema ukosefu wa chakula majumbani unaotokana na uuzwaji wa mazao ya chakula wakati mwingine husababisha ongezeko la watoto wa mitaani kwani watoto hulazimika kwenda mitaani kujitafutia chakula

Bw. Mahenge pia amewataka wananchi hao kutunza mazingira ikiwa ni pamoja na kutunza vizuri mashamba yao mara baada ya kuvuna na kuepuka kuanzisha moto kichaa ambao nao unaharibu mazingira

Akiendelea kuzungumzia suala hilo la utunzaji wa mazingira mwenyekiti huyo pia amewataka wakazi wa Makete kutunza mazingira yao na kuhakikisha yapo katika hali ya usafi muda wote ili kuepukana na uwezekano wa kukumbwa na magonjwa ya milipuko yatokanayo na uchafu uliopo kwenye mazingira wanayoishi

Na Anitha Sanga & Obeth Ngajilo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo