PONGEZI.......

Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Iwawa wilayani Makete Bw. Fredy Chaula pamoja na walimu wa shule hiyo wamepongezwa kwa ushirikiano walioutoa kwa maafisa maendeleo ya jamii wanaofanya mazoezi katika kitengo hicho wakati walipofanya ziara katika shule hiyo

Akizungumza kwa niaba ya wenzake mmoja kati ya maafisa hao Denis Sinene amewapongeza waalimu hao na kuwataka kuonesha ukarimu huo hata kwa watu wengine watakaokuja kuhutaji ushirikiano wao katika kusukuma gurudumu la maendeleo

Katika hatua nyingine maafisa hao wamewataka wazazi na walezi wilayani Makete kufuatilia maendeleo ya watoto wao shuleni, kwani kwa kufanya hivyo watakuwa wamewasaidia waalimu kutatua changamoto za elimu zinazowakabili wanafunzi na taaluma ya elimu itakuwa mwaka hadi mwaka

Amesema wazazi na walezi wakishirikiana pamoja na waalimu watasaidia kupunguza changamoto zinazowakabili wanafunzi ikiwemo utoro shuleni hapo, kwani ni moja ya matatizo yaliyopo katika shule nyingi

Na Obeth Ngajilo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo