Makete

Imeelezwa kuwa ukosefu wa gari kwa ajili ya kuzolea taka wilayani Makete ni moja ya sababu zinazopelekea mlundikano wa taka katika soko la wakulima Makete mjini

Hayo yamesemwa na Afisa Afya wa kata ya Iwawa wilayani hapa Bi. Agatha Mbilinyi wakati akizungumza na waandishi wetu kuhusiana na mlundikano wa taka sokoni hapo

Ameongeza kuwa ubovu wa barabara ya kuelekea lilipo dampo kwa ajili ya kupeleka taka hizo nayo imekuwa chanzo cha mlundikano huo wa taka katika soko hilo

Bi Mbilinyi amesema wakati mwingine wanalazimika kukodi gari la kubebea taka hizo kwa gharama zao wenyewe na wakati mwingine wamiliki wa magari hukataa kwenda kutokana na ubovu wa barabara ya kuelekea dampo hasa kipindi hiki cha masika

Aidha ameiomba halmashauri ya wilaya ya Makete kutenga gari maalum kwa ajili ya kubebea taka hizo kila mara pamoja na kuitengeneza barabara inayoelekea dampo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo