MVUA KUPUNGUA DAR

Mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya hali ya hewa nchini (TMA) Dr. Agnes Kijazi amesema kuanzia leo mvua zilizokuwa zikinyesha jijini DSM na kusababisha mafuriko zitaanza kupungua

Dr. Kijazi amewatoa hofu wakazi wa Dar kuwa mvua hizo zitaanza kupungua baada ya kunyesha kwa kiasi kikubwa kwa muda wa siku mbili mfululizo na kusema kuwa utabiri wao ulikuwa ni mvua kunyesha kwa siku mbili mfululizo, mvua ambazo zingekuwa na madhara makubwa

Wakati huo huo taarifa zilizotolewa na mamlaka ya utabiri wa hali ya hewa kanda ya nyanda za juu kusini hususan mkoa wa Mbeya, mvua kubwa zitanyesha kati ya Disemba 21 - 31 mwaka huu na kusababisha madhara makubwa, hivyo wananchi wachukue tahadhari!


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo