TANESCO KUTOA TATHMINI YA HASARA YA MIUNDOMBINU YAKE ILIYOHARIBIWA NA MAFURIKO BAADAYE


Shirilka la umeme Tanzania (TANESCO) limesema kuwa hadi sasa ni mapema mno kuzungumzia hasara shirika hilo ilizozipata kutokana na miundo mbinu ya umeme kuharibiwa na mafuriko

Hayo yamesemwa na Meneja mahusiano wa shirika hilo Badra Masoud (pichani) wakati akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya shirika hilo kulazimika kukata umeme kwenye maeneo yaliyokumbwa na mafuriko ili kupunguza kutokea kwa madhara zaidi hususan vifo

Baadhi ya hasara shirika hilo ilizozipata ni pamoja na nguzo za umeme kuanguka, transfoma kuanguka pamoja na nyaya kukatika, ila amesema tathmini kamili ya hasara hizo itatolewa baadae na shirika hilo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo