Spika Tulia: Simuogopi Sugu!

Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson amesema ahofii kukabiliana na aliyewahi kuwa Mbunge Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi ‘Sugu,’ endapo watakutana katika kinya’ng’iro cha kugombea jimbo hilo katika uchaguzi mkuu ujao 2025 utakaokuwa huru na haki.


Dk Tulia ametoa msimamo huo leo Mei 4, 2023 wakati akijibu swali katika mahojiano maalumu na runinga moja nchini na kufanyika katika makazi rasmi ya Spika Jijini Dodoma.

Pamoja na mambo mengine, Spika aliuzwa ikiwa hatishiki kukabiliana na Sugu’ katika uchaguzi unaoitwa huru na haki, hasa ikizingatiwa kuwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, wapinzani wengi waliamini kuna nguvu ya ziada ya dola ilitumika kuwabeba walioshinda. Also Read

Pikipiki yalipuka na kuteketea jijini Mwanza Kitaifa 41 min ago Pikipiki yalipuka na kuteketea jijini Mwanza Kitaifa 41 min ago

“Sihofii kupambana naye, niko vizuri sina wasiwasi na hilo naomba Mungu aniweke, nimefanya kazi kubwa, nyie nendeni Mbeya Mjini mtaamini,’ amejinasibu Dk Tulia.

Na akaongeza kusema: “Hata yeye anajua (Sugu), hao wanaojadili mtandaoni nadhani hawajafika Mbeya wala hawapajui wala kuwasikia Mbeya, sasa nyie (waandishi) mnakaribishwa halafu mtawanyike na mkaulize hapa Mbeya Mjini mbunge ni nani, mtapata majibu.”


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo