Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Tarime-Rorya limelazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wananchi waliokuwa wakitaka kumshushia kipigo, Ajuza ambaye jina lake halijafahamika anayekadiriwa kuwa na umri wa zaidi ya miaka 60, wakimtuhumu kuhusika na kupotea kwa watoto watatu kwa njia za kishirikina.
Tukio hilo limetokea wakati Mkuu wa Wilaya hiyo, Juma Chikoka akiwa kwenye kwenye mkutano na wananchi hao, wakijadili tukio la watoto hao ambao wamefanyiwa ukatili ikiwamo kupigwa, kuchomwa moto na kufungiwa ndani kwa muda usiojulikana, ndipo mwanamke huyo aliposikika akiongea na wachawi wenzake juu ya watoto hao, kwa lugha ya kijaluo.