Aliyesababisha vifo vya walevi afikishwa kortini

Mahakama ya Hakimu Mkazi wilaya ya Lindi, imemsomea shtaka moja la mauaji mganga wa kienyeji aitwaye Shigela Ngelanija, anayetuhumiwa kwa kosa la mauaji ya watu watano ambao walimfuata awape dawa ya kunywa ili waache pombe, na baadaye kufariki dunia baada ya kunywa dawa hiyo.


Shtaka hilo amesomewa hii jana Februari 2, 2023, na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo Consolata Singano ambapo mtuhumiwa hakutakiwa kutaja chochote kwa kuwa Mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza kesi hiyo.

Kesi ya Shigela itatajwa tena Februari 15, 2023. Vifo vya watu hao vilitokea Januari 29, 2023, katika Kijiji cha Nambilanje wilaya ya Ruangwa. 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo