Wizara ya Mifugo na Uvuvi licha ya kulaani tukio la kuteketezwa kwa maelfu ya vifaranga wa kuku wa mayai na nyama mkoani Kilimanjaro imesema itachukua hatua za kisheria kwa mwekezaji wa shamba la kuku la Kibo Poultry ili iwe fundisho kwa wengine.
Hatua ya mwekezaji huyo kuteketeza vifaranga hivyo imekuja baada ya kukosekana kwa soko huku ikidaiwa kuwa soko la vifaranga limefurika kutoka nje ya nchi.