Wakamatwa wakisafirisha wanyamapori waliowaua


Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Jeshi la Uhifadhi - TAWA wamefanikiwa kuwakamata watuhumiwa Wanne wakisafirisha wanyamapori aina ya Pundamilia watatu na digidigi mmoja wanaodaiwa kuuwawa katika Pori la Karambandeha lililopo kijiji cha Karambandeha wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro.


Mbali na watuhumiwa hao pia jeshi la Polisi limekamata pikipiki tatu pamoja na mapanga yanayodaiwa kutumika katika ukataji wa nyama huku likieleza linamsaka mtu mmoja ambaye alifanikiwa kutoroka akiwa na silaha aina ya machine gun inayotajwa kutumika katika kuua wanayama hao.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo