Taarifa ya "Majaliwa hakufungua mlango wa ndege" yakanushwa na serikali

Msemaji Mkuu wa serikali Gerson Msigwa amekanusha taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii zikidai ripoti ya uchunguzi wa ajali ya ndege ya Precision Air imetoka na kueleza mambo kadhaa ikiwemo Majaliwa kutofungua mlango wa ndege uliopelekea majeruhi kuokolewa


Msemaji huyo mkuu wa serikali amesema kwamba serikali bado haijatoa taarifa ya uchunguzi wa ajali ya ndege hiyo

"Serikali bado haijatoa taarifa ya uchunguzi wa ajali ya ndege ya kampuni ya Precision air iliyotokea Novemba 6, 2022 huko Bukoba, Taarifa inayosambazwa mitandaoni IPUUZWE kwa kuwa haijatoka katika mamlaka rasmi za serikali, taarifa rasmi itakapokuwa tayari mtajulishwa", - Taarifa ya Msemaji Mkuu wa serikali, Gerson Msigwa.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo