Katika kisa tofauti, mwanamume mmoja mwenye umri wa miaka 48, anapokea matibabu baada ya kushambuliwa na kulawitiwa na genge lisilojulikana katika Kituo cha Nderu eneo la Ndeiya, Kaunti ya Kiambu nchini Kenya.
Uchunguzi umebaini kuwa mwanamume huyo ambaye ni mlemavu, alivamiwa alipokuwa kwa matembezi ya jioni katika eneo la Ndeiya, lilioko kati kati ya kaunti ndogo za Limuru na Kikuyu.
Taarifa zaidi zinasema kuwa mwathiriwa alilawitiwa na wavamizi hao kisha wakamkata sehemu zake za siri.
