Mwenyekiti wa Kijiji atuhumiwa kukamata na kuwahoji wananchi usiku

Wananchi wa kijiji Cha Ilindiwe wilayani Makete mkoani Njombe wamemueleza diwani wao kwamba hawaridhishwi na kitendo cha Mwenyekiti wa Kijiji hicho Laines Sanga kuendesha kesi za watuhumiwa mbalimbali kwenye ofisi ya kitongoji badala ya ofisi ya kijiji waliyoijenga


Pia wananchi hao wamedai kuwa wengine wanakamatwa usiku na kupelekwa ofisi ya kitongoji jambo ambalo Diwani wa kata hiyo Osmund Idawa amelitolea ufafanuzi kwa kuwaambia kwamba kisheria mwenyekiti anaruhusiwa kufanya kazi kwenye ofisi ya kitongoji lakini isiwe mazoea lakini pia aangalie ni jambo gani anatakiwa kulishughulikia usiku akitolea mfano mauaji au wizi
Tazama video hii Mwanzo mwisho



JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo