Muuguzi amchezea densi mgonjwa aliyelazwa hospitalini

Muuguzi  mmoja aligeuka gumzo la siku baada ya kuonekana kwenye kanda ya video akimchangamsha mtoto aliyekuwa mgonjwa kwa ngoma maridadi ikiambatanishwa na densi.


Muuguzi huyo aliyetambuliwa kwa jina  Lukresia Robai alishabikia kwenye mitandao ya kijamii kwa upendo wake aliouonyesha kwa mtoto yule mchanga.


Nesi huyu ambaye pia ni mwanatiktoker alikuwa akimpa tabasabu mtoto yule ambaye angejihisi mpweke kutokana na hali yake ya kulazwa hospitalini.


Mtoto huyo alionekana amejawa na furaha isiyopimika huku akitingiza bega kutokana na mdundo wa ngoma ya "Baby Shark" waliokuwa wakiimbisha.


Densi hiyo iliwafanya watu wengi walioiona kuitazama mara kwa mara nao wengine wakituma msururu wa jumbe ambazo zilionekana kumpongeza muuguzi yule kwa kitendo chake cha huruma na kumpa mtoto furaha sawia na ya mama mzazi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo