Muuguzi mmoja aligeuka gumzo la siku baada ya kuonekana kwenye kanda ya video akimchangamsha mtoto aliyekuwa mgonjwa kwa ngoma maridadi ikiambatanishwa na densi.
Muuguzi huyo aliyetambuliwa kwa jina Lukresia Robai alishabikia kwenye mitandao ya kijamii kwa upendo wake aliouonyesha kwa mtoto yule mchanga.
Nesi huyu ambaye pia ni mwanatiktoker alikuwa akimpa tabasabu mtoto yule ambaye angejihisi mpweke kutokana na hali yake ya kulazwa hospitalini.
Mtoto huyo alionekana amejawa na furaha isiyopimika huku akitingiza bega kutokana na mdundo wa ngoma ya "Baby Shark" waliokuwa wakiimbisha.
Densi hiyo iliwafanya watu wengi walioiona kuitazama mara kwa mara nao wengine wakituma msururu wa jumbe ambazo zilionekana kumpongeza muuguzi yule kwa kitendo chake cha huruma na kumpa mtoto furaha sawia na ya mama mzazi.
