Spika wa Bunge Dk Tulia Ackson ametangaza kuwa Muswada wa Bima ya Afya kwa Wote ambao ulikuwa ujadiliwe bungeni leo Ijumaa umeahirishwa hadi hapo mashauriano kati ya Bunge na Serikali yatakapokamilika.
Spika Amesema kuna mambo ambayo hawajaafikiana na Serikali.
"Muswada huu utaletwa hapa bungeni tutakapokuwa tumemaliza hayo mashauriano” – Spika Tulia Ackson akiahirisha mjadala wa muswada wa sheria ya bima ya afya kwa wote kutokana na mashauriano yanayoendelea kati ya Bunge na Serikali.
