Avua nguo na kutembea Utupu Sokoni ili apewe Elfu 15

Mwanaume mmoja aliyefahamika kwa jina moja tu la Filbert mkazi wa kijiji cha Chibingo Mamlaka ya mji mdogo wa Katoro Mkoani Geita, amewashangaza wananchi wa Kijiji hicho baada ya kuvua nguo na kuanza kutembea uchi maeneo ya sokoni.


Tukio hilo limetokea Novemba 10,2022 ambapo inasemekana alikuwa akibishana na vijana wenzake endapo anaweza kutembea uchi akipewa hela ndipo akavua na kutembea uchi na kulipwa pesa hiyo kiasi cha shilingi 15,000.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Kijiji hicho Bwana Charles Mabuli amesema waliotoa pesa na yeye mwenyewe aliyetembea uchi wote wana makosa na wamedhalilisha jamii ya Chibingo ambapo tayari wamewaadhibu kwa taratibu za jamii ya hapo.
Tazama hapa chini


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo