Ndege ya Precision Air iliyopata ajali wakati wa kutua Bukoba leo ilikuwa imebeba abiria 43 ambapo hadi sasa wameokolewa 26 tu na kupelekwa hospital ya Rufaa ya mkoa Kagera.
Akitoa taarifa ya idadi hiyo Mkoa wa Kagera Albert Chalamila amewaomba wananchi kuendelea kuwa watulivu maana mawasiliano na marubani walioko ndani ya ndege bado yanaendelea.
Ndege hiyo ni ATR 42 yenye namba za usajili 5H BWF ambayo ilikua ikitokea Dar es salaam kuelekea Bukoba na ilikua na safari ya kurudi Dar es salaam kupitia Mwanza.